Thursday, August 1, 2013

LULU AFANYA MSHANGAO KWA JAMII





KUMBE ALIPOTOKA JELA ALIPIGA HODI KWA MAMA KANUMBA!
“Baada ya kutoka jela tu (akiachiwa kwa dhamana) Lulu alikuja nyumbani kwangu na kuniomba msamaha kwa yaliyotokea.
“Niliamua kumsamehe kwa moyo wote, kitu ambacho hakukitegemea.
“Baada ya msamaha huo, nilimkalisha chini na kumshauri kuwa aachane na mambo ya dunia. Nilimwambia yote yaliyotokea Mungu alikuwa na makusudi maalum kwake, ndiyo maana akampitisha kwenye mapito hayo ili abadilike.
“Namshukuru Mungu, baada ya mazungumzo yale Lulu aliamua kubadilika kabisa, amekuwa mtu wa kusoma Biblia. Muda mwingi anautumia kusali. Lulu amekuwa mshauri wangu mkubwa, kila ninapokuwa na jambo linalonikwaza anatumia maneno ya Biblia kunirudisha sawa, anajua sana maneno ya Mungu kunishinda hata mimi. Familia zote mbili (na ya mama Lulu) tunamuombea aendelee hivyohivyo.”
Mama Kanumba hakuishia hapo, alisema kuwa Lulu amekuwa ni mwanaye na ndiye faraja yake kubwa japokuwa Kanumba hayupo tena lakini staa huyo anaendelea kumpenda na kumheshimu kama mama yake.

 Source kimasa

No comments:

Post a Comment